.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 17 Septemba 2016

MANCHESTER CITY YAISHUSHIA KIPIGO BILA HURUMA BOURNEMOUTH

Manchester City imeendeleza ushindi wa nane katika michuano yote kwa msimu huu, baada ya hii leo kupata ushindi laini wa magoli 4-0 dhidi ya Bournemouth katika dimba la Etihad.

Katika mchezo huo Kevin de Bruyne aliwapatia vinara hao wa Ligi Kuu ya Uingereza goli la kwanza kwa shuti la adhabu la chini baada ya Jack Wilshere kufanyiwa madhambi.

City walioutawa mchezo huo walifanikiwa kupata goli la pili kupitia kwa Kelechi Iheanacho na Raheem kuongeza la tatu kabla ya Ilkay Gundogan kufunga kwa utulivu goli la nne.
                  Kelechi Iheanacho akianguka chini baada ya kupiga mpira uliojaa wavuni
                   Raheem Starling akipiga mpira ulioandika goli la tatu la Manchester City

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni