Manchester City imeendeleza ushindi
wa nane katika michuano yote kwa msimu huu, baada ya hii leo kupata
ushindi laini wa magoli 4-0 dhidi ya Bournemouth katika dimba la
Etihad.
Katika mchezo huo Kevin de Bruyne
aliwapatia vinara hao wa Ligi Kuu ya Uingereza goli la kwanza kwa
shuti la adhabu la chini baada ya Jack Wilshere kufanyiwa madhambi.
City walioutawa mchezo huo
walifanikiwa kupata goli la pili kupitia kwa Kelechi Iheanacho na
Raheem kuongeza la tatu kabla ya Ilkay Gundogan kufunga kwa utulivu
goli la nne.
Kelechi Iheanacho akianguka chini baada ya kupiga mpira uliojaa wavuni
Raheem Starling akipiga mpira ulioandika goli la tatu la Manchester City
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni