.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 17 Septemba 2016

ISLAM SLIMANI AJITAMBULISHA RASMI LIGI KUU YA UINGEREZA KWA MAGOLI MAWILI

Mchezaji mpya wa Leicester City aliyesajiliwa kwa rekodi Islam Slimani amecheza mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu na kuifungia timu yake magoli mawili katika ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Burnley.

Mshambuliaji huyo alifunga goli lake la kwanza mnamo dakika ya mwisho ya kipindi cha kwanza kwa kichwa kufuatia mpira wa adhabu uliopigwa na Christian Fuchs.

Slimani alifunga la goli la pili kwa kichwa mara tu baada ya kuanza kipindi cha pili kabla ya Ben Mee kujifunga la tatu baadaye wakati akijaribu kuokoa mpira.
       Islam Slimani akiwa juu angani baada ya kuupiga mpira wa kichwa uliojaa wavuni
                Beki Ben Mee akijifunga goli wakati akijaribu kuokoa krosi ya Mahrez 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni