Utatu mtakatifu katika soka
unaoundwa na Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar umeanza kunoga tena
baada ya wachezaji hao kuisaidia Barcelona kuibuka na ushindi wa
magoli 5-1 dhidi ya timu ndogo ya Leganes katika ligi ya La Liga.
Katika mchezo huo Messi alikuwa wa
kwanza kutikisa nyavu katika dakika ya 15 ya mchezo, na kisha Suarez
kuongeza la pili katika dakika ya 31 baada ya kazi nzuri iliyofanywa
na Messi aliyempasia mpira.
Neymar alifunga goli la tatu katika
dakika ya 44 na baadaye Messi akafunga kwa mkwaju wa penati baada ya
Neymar kufanyiwa madhambi, na kisha Rafinha akafunga goli la tano,
kabla ya Gabriel kuipatia Leganes goli pekee.
Lionel Messi akifurahi baada ya kumpoteza maboya kipa wa Leganes na kuandika goli
Luis Suarez akishangilia goli kwa kumnyooshea kidole Lionel Messi aliyempasia pasi
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni