.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 17 Septemba 2016

MESSI, SUAREZ NA NEYMAR WAISAMBARATISHA LEGANES KATIKA LA LIGA

Utatu mtakatifu katika soka unaoundwa na Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar umeanza kunoga tena baada ya wachezaji hao kuisaidia Barcelona kuibuka na ushindi wa magoli 5-1 dhidi ya timu ndogo ya Leganes katika ligi ya La Liga.

Katika mchezo huo Messi alikuwa wa kwanza kutikisa nyavu katika dakika ya 15 ya mchezo, na kisha Suarez kuongeza la pili katika dakika ya 31 baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Messi aliyempasia mpira.

Neymar alifunga goli la tatu katika dakika ya 44 na baadaye Messi akafunga kwa mkwaju wa penati baada ya Neymar kufanyiwa madhambi, na kisha Rafinha akafunga goli la tano, kabla ya Gabriel kuipatia Leganes goli pekee.
   Lionel Messi akifurahi baada ya kumpoteza maboya kipa wa Leganes na kuandika goli
   Luis Suarez akishangilia goli kwa kumnyooshea kidole Lionel Messi aliyempasia pasi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni