.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 5 Septemba 2016

AUWSA YAJA NA RASIMU YA MABORESHO YA HUDUMA KWA MTEJA

Mgeni Rasmi ambaye alimwakilisha mkuu wa wilaya ya Arusha Afisa Tarafa wa jiji la Arusha Felician Rutahengerwa akisoma hotuba hiyo mbele ya wadau wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira jijini Arusha leo kushoto ni mwenye miwani ni Mkurugenzi wa Auwsa Ruth Koya na kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya Auwsa Job Laizer na mjumbe wa bodi hiyo wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi kwenye mkutano wa Maboresho ya rasimu ya mkataba wa huduma za mteja,picha zote na mahmoud ahmad wa michuzi blog arusha
Wadau mbali mbali waliopata nafasi ya kushiriki katika mkutano wa maboresho ya huduma kwa mteja wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi hayupo pichani katika viwanja vya makumbusho jijini Arusha leo
Mkurugenzi wa Auwsa Ruth Koya akiongea na kujibu maswali ya wadau wa mamlaka hiyo na wakazi wa jiji la Arusha juu ya maboresho ya rasimu ya huduma kwa mteja leo jijini Arusha picha na mahmoud Ahmad wa michuzi blog Arusha
Baadhi ya wadau na wakazi wa jiji la Arusha wakifuatilia majibu ya mkurugenzi juu ya uboreshaji wa huduma kwa mteja kwenye viwanja vya makumbusho jijini Arusha

Maafisa wa kitengo cha Mawasiliano na uhusiano wa Mamlaka hiyo wakiwa wanaratibu shughuli hiyo kama walivyokuwatwa na kamera ya matukio ya michuzi blog jijini Arusha leo
Maafisa wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira wakiandika maelezo na malalamiko mbali mbali yaliotolewa na wadau wa Auwsa pamoja na wakazi wa jiji la Arusha
Wakazi mbali mbali wa jiji la Arusha walioshiriki mkutano huo wa maboresho ya rasimu ya huduma kwa mteja picha juu na chini
WAfanyakazi wakiwa kazini kuratibu shughuli hiyo ya maboresho ya rasimu ya huduma kwa mteja picha zote na mahmoud ahmad wa Michuzi blog Arusha. 
  
                                                                                         Na MahmoudAhmad Arusha

Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingiza imewataka wakazi wa jiji la Arusha kukaa mkao wa kula kwani wapo katika wakati wa kuboresha huduma zake kwenye kipindi cha miaka miwili na nusu iliyobakia katika uboresha wa miundombinu na utafutaji wavyanzo vipya vya maji na kuwa tatizo la maji litakuwa historia.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa AUWSA Ruth Koya wakati akijibu maswali ya wadau mbali mbali walioshiriki kwenye Mkutano wa maboresho ya mkataba wa huduma kwawateja jijini Arusha.Alisema kuwa kumekuwa na matatizo ya upungufu wa maji kwa mda mrefu na serikali imeliona
hilo ndio maana ikatenga kiasi cha tsh,476 bilion za uboreshaji wa huduma mbali mbali za mamlaka hiyo hivyo suala hilo linafanyiwa kazi kuanzia mwaka huu hadimwaka 2018 litakapokamilika.


“Tuwe na subra maradi huu kwa sasa una mda wa miezi nane tangia uanze na mkandarasi wa utafutaji wa vyanzo vya maji yupo kazi akishakamilisha tutaanza maboresho yamiundombinu yetu ilkuweza kuwafikishia maji kwa wateja wetu wote”alisema Koya. 

Kwa upande wake kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Arusha Afisa tarafa wa jiji la Arusha Felician Rutehengerwa aliitaka Auwsa kuwabainisha wezi wote wa maji ilikuweza kuwafisha katika mikono ya kisheria kwani suala hilo pia linachangia wananchikukosa huduma ya maji safi na upotevu wa maji.

Alisema kuwa kumekuwapo na vyanzo vingi vya maji zaidi ya 19 na vingine vimeanzishwa na viwanda ambavyo vimekuwa vikiikosesha Auwsa mapato ikiwemo kiwanda cha A to Z ambacho kimekuwa kikigawa maji bure
huku wakitambua kuwa wao hawana mamlaka ya kisheria ya usimamizi wa maji hivyoni mteja mkubwa mnampoteza kulipa huduma za maji.


Nae Mwenyekiti wa Bodi ya Auwsa Job Laizer alisema kuwa Malalamiko ambayo wananchi wameyatoa ni changamoto kubwa kwao katika kuifanya mamlaka hiyo kuboresha huduma zake na kuwaahidi wadau kuyasimamia na kuahkikisha wateja wanapatahuduma bora na kwa wakati.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni