Muigizaji filamu Brad Pitt amesema
ameshtushwa na hatua ya mkewe Angelina Jolie kuwasilisha nyaraka za
kudai talaka, na ameomba kuwepo na usiri ili kutowaathiri watoto wao.
Akiongea na gazeti la People Pitt
amesema kuwa ameshutushwa na uamuzi huo wa mkewe, ila cha muhimu sasa
ni mustakabali wa watoto wao.
Muigizaji filamu Jolie, 41,
amewasilisha nyaraka za kudai talaka kutoka kwa Pitt, 52, kwa madai
ya kuwepo kwa tafauti baina yao ambazo haziwezikupata usuluhishi.
Brad Pitt na Angelina Jolie wakiwa na familia yao
Muigizaji Mfaransa Marion Cotillard anayedaiwa kutibua ndoa ya Pitt na Jolie akiwa na mwenza wake Guillaume Canet
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni