Romelu Lukaku amepachika magoli
mawili kwa kichwa wakatia Ubelgiji ikipata ushindi wa magoli 3-0
dhidi Cyprus, ikiwa ni ushindi wa kwanza kwa kocha mpya Roberto
Martinez, katika mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya kombe la dunia
2018.
Mchezaji Yannick Carrasco aliongeza
goli la tatu baada ya Lukaku kufunga magoli mawili yote kwa kichwa,
na kuifanya Ubelgiji kuanza kuonyesha kuwa na uwezo wa kuongoza kundi
lao licha ya kutofanya vyema kwenye michuano ya Euro 2016.
Romelu Lukaku akishangilia kwa kukimbia baada ya kufunga goli huku Fellaini akiwa nyuma yake
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni