.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 13 Septemba 2016

KILIMANJARO QUEENS YAANZA NA USHINDI KOMBE LA CHALENJI

Timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Queens, jana ilianza vyema mashindano ya Kombe la Chalenji baada ya kuifunga Rwanda kwa magoli 3-2 katika mchezo uliofanyija Jinja, Uganda.

Katika mchezo huo Kilimanjaro Queens waliandika goli la kwanza katika dakika ya 11 kupitia kwa Asha Rashid na kisha baadaye ilifunga la pili katika dakika ya 28 mfungaji akiwa ni Stumai Abdallah.

Rwanda walipata goli lao la kwanza kupitia kwa Ibangarrye Marie, na hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, Kilimanjaro Queens walikuwa mbele kwa mabao 2-1. Katika kipindi cha pili, Kilimanjaro walijifunga kwa goli la Amona Ally na matokeo kuwa 2-2.

Rashid alifunga bao lake la pili na kuiwezesha Kilimanjaro Queens kupata goli la tatu katika dakika ya 65.

Katika mechi za ufunguzi juzi, wenyeji Uganda walitoa kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa Kenya, huku Zanzibar ikipokea kichapo cha mbwa mwizi kutoka kwa Burundi baada ya kufungwa magoli 10-0 katika mchezo mwingine wa Kundi A.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni