Mtawa Mama Teresa, ambaye
anajulikana zaidi kwa kujitolea katika kuwasaidia masikini nchini
India, atatangazwa kuwa mtakatifu hii leo Jijini Vatican.
Makumi kwa melfu ya watu
wamekusanyika katika eneo lawazi la Kanisa la Mtakatifu Peter
kushuhudia Papa Francis akiongoza hafla hiyo ya kutangazwa Mtakatifu
Mama Teresa.
Kuridhiwa utakatifu wa Mama Teresa
kunafuatia ushuhuda wa miujiza miwili ya kutibu wagonjwa aliyofanya
Mama Teresa, baada ya kifo chake.
Watu 1,500 wasio na makazi nchini
Italia wamepelekwa kwa mabasi Jijini Roma kushuhudia hafla hiyo, na
watapatia mlo wa mchana wa pizza na watawa 250 wa Taasisi ya Masista.
Watawa wa Taasisi ya Mama Teresa wakiwasili Vatican
Watawa wa Taasisi ya Mama Teresa wakiwasili Vatican
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni