Basi la abiria pamoja lori la mafuta
yamegongana kusini mwa Afghanistan, na kusababisha vifo vya watu 36.
Basi hilo lilikuwa likisafiri kutoka
Kandahar kwenda Kabul wakati ajali hiyo ikitokea katika eneo la
Jildak mkoani Zabul.
Wengi waliokufa, wamo wanawake na
watoto, ambapo watu wameungua kiasi cha kushindwa kutambulika. Watu
wengine 25 pia wamejeruhiwa.
Nchi ya Afghanistan imekuwa na ajali
mbaya za barabarani, ambapo barabara nyingi ziko katika hali mbaya na
magari ni mabovu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni