.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 6 Septemba 2016

NCHI YA SUDANI KUSINI YAINGIA RASMI KUWA MWANACHAMA WA EAC

Na Woinde Shizza,Arusha

Nchi za jumuiya wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki chini ya mwenyekiti wa nchi hizo Dr John Pombe Magufuli hii leo wamepokea hati ya udhibitisho wa nchi ya Sudani Kusini kuwa miongoni mwa nchi wanachama wa jumuiya hiyo.

Awali mapema mwaka huu walitia saini makubaliano ya kutaka kujiunga na kuwa mmoja wan chi jumuiya wanachama ambapo wataalamu kutoka nchi wanachama ambapo Rais Magufuli ndiye mwenyekiti kiongozi wa jumuiya hiyo walizingatia vigezo na masharti vya kuwa mwanachama wa jumuiya hiyo ambapo leo hii yamekamilika.

Awali akizungumza mbele ya wajumbe kutoka sudani kusini katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika Mashariki Liberat Mfumukeko alisema kuwa jumuiya hiyo imepokea hati ya uthibitisho wa wanachama wapya wa jumuiya ya Afrika mashariki na kwamba wanasubiri Mwenyekiti John Magufuli kuidhinisha rasmi katika Mkutano wa wakuu wa nchi unaotarajiwa kufanyika jijini Daresalaam septemba 8 mwaka huu.

Kwa upande wake Mshauri wa Rais wa Sudan kusini katika masuala ya Kiuchumi Aggrey Tisa Sabun ambapo alisema kuwa wamekuwa wakitamani muda mrefu kuwa nchi wanachama na kwamba kuleta hati ya maakubaliano ni hatua moja wapo ya muunganiko huo.

Nao Alex mushi na Vailet mushi wanajumuiya ya Afrika mashariki wanasema kuwa Sudani Kusini Kujuinga na jumuiya hiyo ina faida mbalimbali ikiwemo masuala ya uchumi lakini pia nchi za jumuiya zinapaswa kufikiri Zaidi na kumaliza machafuko ambayo yanaendelea katika nchi hiyo kwani hali hiyo inatia ho

Nae Waziri wa mambo ya nje ushirikiano wa Kimataifa Agustine Maiga ambapo alisema kuwa wamepokea nyaraka hizo kwa niaba ya Mwenyekiti Rais Magufuli na kwamba hivi sasa wanaruhusiwa kushiriki katika vikao vyote kuanzia sasa na wamekuwa wanachama rasmi wa jumuiya hiyo na watapata fursa mbalimbali kama nchi mwanachama.

Kutokana na Sudan ya Kusini kuingia rasmi katika jumuiya hiyo ipo haja ya nchi kuendelea kuwa wamoja na kwamba waweze kukaa pamoja na kutatua changamoto na machafuko yaliyoko katika nchi hizo , ikiwemo kutafuta ufumbuzi wa mapigano nchini humo na kuwezesha wanajumuiya kutafuta fursa za kibiashara nchini humo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni