Mchezaji
Mnaigeria Nwankwo Kanu akitokea benchi ameifungia timu ya wachezaji
wazamani wa wakongwe wa Arsenal magoli 3, katika ushindi wa magoli
4-2 dhidi ya wenzao wa AC Milan.
Hata
hivyo Kanu ambaye alidhani kuwa amepangwa katika kikosi kinachoanza
alijikuta akilazimika kutoka uwanjani baada ya kuingia kuanza
kimakosa, huku Gilberto Silva akimpa tafu kutoka uwanjani.
Baada
ya kuingia akitokea benchi Kanu alionekana kutulia mno licha ya
kuwa na umri wa miaka 40, alifunga goli la kwanza kwa kichwa, na kisha
kuongeza la pili kwa kichwa na goli la tatu alifunga kwa mkwaju wa
penati.
Gilberto Silva akimpa tafu Kanu kutoka nje ya uwanja baada ya kungundua hajapangwa kuanza kucheza mwanzo wa mchezo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni