.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 3 Septemba 2016

NWANKWO KANU AIFUNGIA ARSENAL MAGOLI 3 KATIKA MCHEZO WA WAKONGWE

Mchezaji Mnaigeria Nwankwo Kanu akitokea benchi ameifungia timu ya wachezaji wazamani wa wakongwe wa Arsenal magoli 3, katika ushindi wa magoli 4-2 dhidi ya wenzao wa AC Milan.

Hata hivyo Kanu ambaye alidhani kuwa amepangwa katika kikosi kinachoanza alijikuta akilazimika kutoka uwanjani baada ya kuingia kuanza kimakosa, huku Gilberto Silva akimpa tafu kutoka uwanjani.

Baada ya kuingia akitokea benchi Kanu alionekana kutulia mno licha ya kuwa na umri wa miaka 40, alifunga goli la kwanza kwa kichwa, na kisha kuongeza la pili kwa kichwa na goli la tatu alifunga kwa mkwaju wa penati.
Gilberto Silva akimpa tafu Kanu kutoka nje ya uwanja baada ya kungundua hajapangwa kuanza kucheza mwanzo wa mchezo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni