Rais
Robert Mugabe wa Zimbabwe amekebehi uvumi wa hivi karibuni kuhusu
afya yake, kwa kusema kwa mzaha kwamba alikufa na kisha kufufuka.
Mugabe,
92, ametoa kauli hiyo ya mzaha, wakati alipowasili kutoka nje katika
uwanja wa ndege wa Harare akiwa kwenye hali ya uchangamfu wakati
akishuka kwenye ndege.
Safari
yake ya ndege ilikuwa ielekea Asia ya Mashariki, lakini badala yake
alienda Dubai, ambapo amesema alienda huku kwa masuala ya kifamilia.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni