Rais
Uhuru Kenyatta leo amepuuzia ripoti za vyombo vya habari vya Kenya
zinazoashiria kuwepo kwa mgogoro baina ya Kenya na Tanzania.
Akiongea
wakati akizindua temino ya pili katika bandari ya Mombasa, rais
Kenyatta amekanusha kuwepo kwa aina yoyote ya mgogoro, na kusema nchi
hizo zinategemeana.
“Nimesoma
magazeti na kuangalia televisheni zikiashiria kuwepo mgogoro baina
yetu, lakini nataka kuwaeleza wazi kuwa Kenya na Tanzania hazipo
kwenye mgogoro wa aina yoyote,” alisema Kenyatta.
Rais
Kenyatta amesema uchumi wa mataifa haya mawili unaingiliana na ni kwa
manufaa ya wananchi wa Kenya na Tanzania.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni