.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 5 Septemba 2016

STARTIMES KUONYESHA MICHUANO YA ULAYA KUWANIA KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2018

                                                                                            Na Dotto Mwaibale

MATAIFA 54 ya Barani Ulaya siku ya Jumapili hii yatashuka dimbani katika harakati za kuwania nafasi ya kufuzu ili kuungana na mwenyeji nchi ya Urusi katika michuano ya kombe la dunia itakayofanyika nchini humo mwaka 2018.

Akitoa taarifa hiyo ya kusisimua kwa mashabiki wa soka nchini Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Zuhura Hanif amesema kuwa hii ni habari njema kwa wateja wetu na watanzania kwani wataweza kufuatilia kwa ukaribu kabisa mechi zote moja kwa moja kwenye runinga zao.

“Michuano ya kuwania tiketi ya kufuzu kwenye kombe la dunia itakayofanyika nchini Urusi mwaka 2018 kwa nchi za Ulaya itakuwa ni yenye ushindani mkubwa ukizingatia ubora wa timu na wachezaji wake. Kwenye michuano hii mashabiki wataweza kujionea moja kwa moja mabingwa watetezi Ujerumani watakapoanza safari yao ya kulitetea kombe hilo kwa kuvaana na Norway.

Pia macho ya wapenzi wengi wa soka watapenda kuiona Uingereza ikiwa chini ya kocha wake mpya Sam Allardyce watakaposhuka dimbani kucheza na Slovakia.” Alisema Hanif

“StarTimes inayofuraha kuwataarifu watanzania kwamba mechi zote za michuano hii zitaonekana moja kwa moja kupitia chaneli zetu mahususi kabisa za michezo ambazo ni Sports Focus, Sport Arena, World Football, Sport Arena na Sport Premium.

Tunafahamu ya kwamba soka ni mchezo unaopendwa sana hapa nchini, na sisi tupo katika kuhakikisha kuwa hilo linawezekana kwa gharama nafuu kabisa.” Aliongezea Hanif

Mabingwa wa kombe la EURO mwaka 2016 timu ya Ureno nayo itashuka dimbani siku ya Jumatatu ya Septemba 5 kwenye mchezo wa kundi B dhidi ya Uswisi jijini Basel bila ya nahodha wake Christiano Ronaldo ambaye bado anauguza jeraha la goti ambalo lilimfanya atolewe kwenye kipindi cha kwanza kwenye fainali za EURO zilizofanyika nchini Ufaransa.

“Michezo na burudani ni maudhui ambayo tunayatilia sana maanani StarTimes na ndiyo maana kila kukicha tunazidi kuongeza zaidi. Wateja wetu kwa malipo ya gharama nafuu kabisa ya mwezi wataweza kutazama mechi zote za michuano hii moja kwa moja kwenye chaneli tano tulizonazo mahususi kwa michezo pekee.

Ninawaomba watanzania kuichangamkia hii fursa kwa kujiunga nasi na kufurahia kwa pamoja mchezo wa soka kupitia visimbuzi vyetu,” alihitimisha Hanif.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni