.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 18 Septemba 2016

TIMU YA MANCHESTER UNITED YAPATA KIPIGO CHA TATU MFULULIZO

Timu ya Manchester United imejikuta ikipata kipigo cha tatu mfululizo baada ya kufundishwa soka na Watford na kukubali kipigo cha magoli 3-1 katika dimba la Vicarage Road.

Baada ya kupoteza mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Manchester City, na kisha baadaye wa Ligi ya Uropa dhidi ya Feyenoord, kikosi cha Jose Mourinho kimepata kipigo tena hii leo.

Katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya Uingereza, Etienne Capoue, aliifungia Watford goli la kwanza kabla ya Marcus Rashford kusawazisha.

Hata hivyo, Juan Camilo Zuniga akitokea benchi alifunga goli la pili baada ya kuugusa mpira kwa mara ya kwanza na kisha Troy Deeney akifunga la tatu kwa mkwaju wa penati.
                                                Etienne Capoue akiifungia Watford goli la kwanza 
                               Marcus Rashford akifunga goli pekee la Manchester United

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni