Timu ya Manchester United imejikuta
ikipata kipigo cha tatu mfululizo baada ya kufundishwa soka na
Watford na kukubali kipigo cha magoli 3-1 katika dimba la Vicarage
Road.
Baada ya kupoteza mchezo wa Ligi Kuu
dhidi ya Manchester City, na kisha baadaye wa Ligi ya Uropa dhidi ya
Feyenoord, kikosi cha Jose Mourinho kimepata kipigo tena hii leo.
Katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya
Uingereza, Etienne Capoue, aliifungia Watford goli la kwanza kabla ya
Marcus Rashford kusawazisha.
Hata hivyo, Juan Camilo Zuniga
akitokea benchi alifunga goli la pili baada ya kuugusa mpira kwa mara
ya kwanza na kisha Troy Deeney akifunga la tatu kwa mkwaju wa penati.
Etienne Capoue akiifungia Watford goli la kwanza
Marcus Rashford akifunga goli pekee la Manchester United
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni