Diego Costa ameondoa ukame wa magoli
katika michezo ya kimataifa baada ya kuitwa kwenye timu ya taifa,
wakati Hispania ikiichakaza Liechtenstein magoli 8-0 katika mchezo wa
kuwania kufuzu michuano ya kombe la dunia.
Katika mchezo huo Diego Costa
aliandika goli la kwanza na baadaye beki Sergi Roberto aliifungia
Hispania goli la pili, Silva alifunga goli la tatu, Vitolo la nne,
Diego Costa la tano Morata la sita na la saba na Silva kumalizia la
nane.
Mchezaji David Silva akiufuata wavuni mpira baada ya kufunga goli
Beki Sergi Roberto akiachia shuti lililojaa wavuni na kuandika goli
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni