Timu ya Wales imeanza kampeni ya
kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2018 kwa kujiamini baada ya
kupata ushindi wa kishindo wa magoli 4-0 dhidi ya Moldova.
Katika mchezo huo Wales walikumbana
na upinzani mkali kutoka kwa Moldovan, lakini walipambana vikali na
kuongoza kwa magoli 2-0 hadi kufikia mapumziko kupitia magoli ya
Sam Vokes na Joe Allen.
Mchezaji nyota wa kutegemewa wa
Wales na Real Madrid Gareth Bale alifunga goli la tatu na kisha
kufunga goli la penati katika dakika za mwisho.
Mchezaji tegemeo wa Wales gareth Bale akifunga goli
Mshambuliaji wa Burnley Sam Vokes akishangilia goli aliloifungia Wales
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni