TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: KUKANUSHA TAARIFA INAYOSAMBAZWA
KWENYE MITANDAO MBALIMBALI YA KIJAMII
Ofisi ya Makamu wa Rais inakanusha
taarifa inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan,
ameomba kujiuzulu nafasi yake na kwamba taarifa hiyo ni ya uzushi na
uongo haina ukweli wowote.
Taarifa hiyo ni ya uchochezi
inayolenga kuliweka Taifa kwenye taharuki. Mhe. Makamu wa Rais yuko
bega kwa bega na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika
kufanya kazi zao kwa mujibu wa Katiba ya nchi ili kuwaletea wananchi
maendeleo.
Ofisi ya Makamu wa Rais inawataka
wananchi na Watanzania kwa ujumla kupuuza taarifa hiyo ambayo
inalenga kupotosha umma kuhusu ushirikiano mzuri uliopo baina ya
Viongozi wetu.
Mwisho, Ofisi ya Makamu wa Rais
inawasihi Watanzania kufanya kazi kwa bidii na wajiepushe na vitendo
vinavyolenga kuvuruga amani na utulivu nchini.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es Salaam
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni