.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 22 Septemba 2016

VILLARREAL YATIBUA MIPANGO YA REAL MADRID KUWEKA REKODI

Real Madrid imepoteza nafasi ya kuvunja rekodi ya kushinda michezo 17 mfululizo katika Ligi ya La Liga baada ya kulazimishwa sare ya goli 1-1 na Villarreal.

Wenyeji Madrid walijikuta wakifungwa goli baada ya Sergio Ramos kuuzuia kwa mkono mpira na Bruno Soriano kufunga kwa mkwaju wa penati.

Hata hivyo baadaye Sergio Ramos alirekebisha makosa yake baada ya tu ya kuanza kipindi cha pili kwa kufunga kwa kichwa mpira wa kona.
                Sergio Ramos akiwa ameupiga mpira kwa kichwa ambao ulienda kujaa wavuni
                     Cristiano Ronaldo alidhibitiwa vilivyo na kushindwa kutikisa nyavu
 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni