.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 22 Septemba 2016

MTUKUTU MARIO BALOTELLI AENDELEA KUTAKATA NCHINI UFARANSA

Mwanzo mzuri wa Mario Balotelli akiwa na klabu ya Nice umeendelea baada ya mchezaji huyo kutundika magoli mawili wakati wakiizamisha Monaco kwa magoli 4-0 katika mchezo wa Ligi 1.

Mshambuliaji huyo raia wa Italia alifunga magoli mawili katika mchezo wake wa kwanza tangu ahamie Ligi ya Ufaransa, na jana tena alifumania nyavu katika vipindi vyote viwili.

Magoli mengine ya Nice yalifungwa na Paul Baysse aliyefunga la kwanza, huku Alassane Plea akikamilisha la nne na kuifanya Nice kuchuma pointi 14 katika michezo sita.
                                               Mario Balotelli akiachia shuti na kuandika goli

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni