Wanawake watatu wameuwawa Kenya
baada ya kujaribu kufanyashambulizi katika kituo kikuu cha polisi
katika mji wa Mombasa.
Wanawake hao waliokuwa wamevalia
vazi la hijabu, waliingia katika kituo hicho cha polisi wakisema
wanataka kuripoti tukio la kuibiwa simu.
Katika tukio hilo mwanamke mmoja
alichomoa kisu, na mwingine alitupa bomo la petroli na kusababisha
moto ambapo katika tukio hilo maafisa polisi wawili walijeruhiwa.
Haijafahamika nani haswa amehusika
na shambulizi hilo, hata hivyo kundi la wapiganaji wa al-Shabab
limekuwa likifanya mashambulizi nchini Kenya.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni