Mgombea urais wa Marekani Bi.
Hillary Clinton, amefuta safari yake ya kwenda California, baada ya
kubainika kuugua ugonjwa wa nimonia.
Bi. Clinton aliugua jana katika
tukio la kumbukumbu ya Septemba 11, na kulazimika kuondoka huku
akishikiliwa na walinzi na aliishiwa nguvu na kutaka kuanguka.
Daktari wake Dk. Lisa R Bardack
amesema jana usiku kuwa Bi. Clinton alipandwa na joto kali na
kuishiwa na maji mwilini akiwa katika kumbukumbu za tukio hilo huko
Manhattan.
Bi. Hillary Clinton akisaidiwa na wasaidizi wake kwenda kwenye gari lake
Bi. Hillary Clinton akikaribia kuanguka baada ya kuishiwa nguvu alipokaribia gari lake
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni