.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 8 Oktoba 2016

CRISTIANO RONALDO ATUPIA NNE WAVUNI WAKATI URENO IKIFANYA MAUAJI

Cristiano Ronaldo amecharuka na kufunga magoli manne kwa timu yake ya taifa ya Ureno wakati ikiiangushia kipigo kizito Andorra cha magoli 6-0 katika mchezo wa kuwania kufuzu kutinga kombe la dunia mwaka 2018.

Cristiano Ronaldo alifunga mara mbili kwa kichwa katika dakika nne za kwanza za mchezo huo na kuwafanya mabingwa hao wa Euro 2016 kutawala mchezo huo.

Joao Cancelo aliifungia Ureno goli la tatu na kisha baadaye Ronaldo kufunga la nne katika dakika ya 42 na kufikisha hat trick yake ya 42 katika rekodi yake ya uchezaji soka.

Ronaldo alifumania nyavu tena na pia Andre Silva akafunga goli la sita katika mchezo huo ulioshuhudia wachezaji wawili wa Andorra wakitolewa nje kwa kadi nyekundu.
                          Cristiano Ronaldo akifunga goli la kwanza kwa mpira wa kichwa 
                             Cristiano Ronaldo akifunga goli lingine kwa mpira wa kichwa
                  Cristiano Ronaldo akifunga goli la tatu kwa shuti alilopiga kitaalam 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni