.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 8 Oktoba 2016

WACHEZAJI WA LIGI KUU YA UINGEREZA WAITAKATISHA UBELGIJI

Eden Hazard, Romelu Lukaku na Toby Alderweireld wameifungia Ubelgiji na kuisaidia kuibuka na ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya Bosnia, katika mchezo wa kuwania kufuzu kutinga fainali za kombe la dunia 2018.

Katika mchezo huo Ubelgiji walipata goli la kwanza kufuatia goli la kujifunga la Emir Spahic, ambaye alijikuta akitumbukiza mpira wavuni katika harakati za kuuokoa.

Eden Hazard aliongeza goli la pili baada ya kumzungusha kipa Asmir Begovic na kisha Toby Alderweireld akaongeza la tatu kwa mpira wa kisigino na Lukaku akakamilisha goli la nne.
                                 Eden Hazard akimpiga chenga kipa Begovic na kufunga goli 
                 Romelu Lukaku akiachia shuti lililojaa wavuni na kuandika goli la nne 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni