.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 23 Oktoba 2016

KAPTENI WA BARCELONA ANDRES INIESTA NJE YA UWANJA KWA WIKI SITA

Kapteni wa Barcelona, Andres Iniesta, atakuwa nje ya uwanja kwa wiki sita baada ya kuumia goti katika mchezo ambao waliibuka na ushindi wa dakika za mwisho dhidi ya Valencia.

Kiungo huyo wa Barcelona aliumia baada ya kukabwa na Enzo Perez baada ya dakika 14 za mchezo walioshinda kwa magoli 3-2 na kutolewa nje kwa machela.

Iniesta atakosa michezo yote ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi, na ni dhahiri sasa hatoshuka dimbani kuivaa Manchester City Novemba mosi.
              Andres Iniesta akiwa chini akipiga kelele kwa maumivu baada ya kuumia goti
  Iniesta akiwa amewekwa kwenye machela ili kusaidiwa kutoka uwanjani baada ya kuumia goti

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni