.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 23 Oktoba 2016

LIVERPOOL YASHINDWA KUONGOZA LIGI LICHA YA KUIFUNGA WEST BROM

Liverpool imepata ushindi wa 2-1 dhidi ya West Brom, lakini wakaruhusu kufungwa goli la dakika za mwisho na kuwanyima nafasi ya kuongoza msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Kikosi hicho cha Jurgen Klopp kiliutawala mchezo huo katika dimba la Anfield na kupata goli la kwanza kupitia kwa Sadio Mane aliyeunganisha krosi ya Roberto Firmino.

Philippe Coutinho alifunga goli la pili akiunasa mpira uliopigwa na Mane, hata hivyo beki Gareth McAuley alichomoa goli moja baada ya Liverpool kushindwa kuokoa mpira wa kona.
                            Sadio Mane akipiga mpira na kufunga goli la kwanza la Liverpool
   Philippe Coutinho akipiga mpira uliomshinda kipa Ben Foster na kuandika goli la pili

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni