Mfungwa aliyeachiwa huru kwa
masamaha wa rais Uhuru Kenyatta wiki iliyopita amefikishwa mahakamani
jana akikabiliwa na tuhuma za kuiba sadaka kanisani.
Mtuhumiwa huyo, Lucas Ngugi Njoroge,
amefikishwa katika Mahakama ya Nyahururu mbele ya Hakimu Judith
Wanjala.
Njoroge aliachiwa huru kutoka gereza
la Nyahururu GK, siku ya Ijumaa baada ya rais Kenyatta kutoa msamaha
kwa wafungwa siku ya Mashujaa.
Mtuhumiwa Njoroge ameshtakiwa kuwa
Oktoba 23, aliiba shilingi 900 za Kenya fedha za sadaka katika Kanisa la Ol Jabet
African Independent Pentecostal huko Laikipia Magharibi, kaunti
Laikipia.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni