.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 25 Oktoba 2016

MFUNGWA ALIYEACHIWA KWA MSAMAHA WA RAIS WIKI ILIYOPITA AKAMATWA KWA KUIBA SADAKA

Mfungwa aliyeachiwa huru kwa masamaha wa rais Uhuru Kenyatta wiki iliyopita amefikishwa mahakamani jana akikabiliwa na tuhuma za kuiba sadaka kanisani.

Mtuhumiwa huyo, Lucas Ngugi Njoroge, amefikishwa katika Mahakama ya Nyahururu mbele ya Hakimu Judith Wanjala.

Njoroge aliachiwa huru kutoka gereza la Nyahururu GK, siku ya Ijumaa baada ya rais Kenyatta kutoa msamaha kwa wafungwa siku ya Mashujaa.

Mtuhumiwa Njoroge ameshtakiwa kuwa Oktoba 23, aliiba shilingi 900 za Kenya fedha za sadaka katika Kanisa la Ol Jabet African Independent Pentecostal huko Laikipia Magharibi, kaunti Laikipia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni