Bingwa wa uzito wa juu wa IBF
Muingereza, Anthony Joshua, hatopigana tena na Wladimir Klistchko
mwaka huu.
Mabondia hao walikuwa wapigane
Desemba 10, lakini Klitschko amepata majeraha madogo wakati akifanya
mazoezi.
Sasa Joshua atapanda ulingoni
Desemba 10 kupigana na David Prince, huku pambano lao na Klitschko
likitarajiwa kufanyika mwezi Machi ama Aprili mwakani.
Bingwa wa IBF Muingereza Anthony Joshua akiwa na mkanda wake
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni