.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 24 Oktoba 2016

NABII MALISA AHUBIRI KATIKA MKUTANO WA INJILI JIJINI ARUSHA

Kiongozi mkuu wa kanisa la Ukombozi ,Nabii B.G Malisa akihubiri katika mkutano mkubwa wa maombezi wa siku 8 katika viwanja vya reli jijini Arusha ambapo amewatakaWatanzania kudumisha amani ya nchi kwa kuepuka kufanya matukio ambayo yanaweza kuchochea vurugu na hatari ya kuliingiza taifa katika hali ya machafuko. (Picha na Pamela Mollel)
Watu mbalimbali waliojitokeza katika mkutano wa Kiongozi mkuu wa kanisa la Ukombozi ,Nabii B.G Malisa unaofanyika katika viwanja vya reli jijini Arusha

                                                                                                        Pamela Mollel,Arusha
 

Watanzania wametakiwa kudumisha amani ya nchi kwa kuepuka kufanya matukio ambayo yanaweza kuchochea vurugu na hatari ya kuliingiza taifa katika hali ya machafuko.

Wito huo umetolewa jana na mchungaji kiongozi wa kanisa la Ukombozi hapa nchini, Nabii B. G Malisa wakati alipokuwa akihubiri neno la Mungu katika viwanja vya reli jijini Arusha na kuhudhuriwa na maelfu ya watu

Nabii Malisa alisema kwamba watanzania wana jukumu kubwa la kuhakikisha wanaombea amani ya nchi iendelee kutawala kwa kuwa bila amani hakuna kitu kitakachoweza kuendelea katika nchi hii

Aidha alisema kuwa amekuwa akifanya ziara mbalimbali katika nchi mbalimbali duniani na kushuhudia hali ya usalama ikiwa tete ambapo askari wamekuwa wakitembea mitaani huku wameshika silaha za moto.

"Hivi karibuni nilikuwa Nigeria wakati nashuka uwanja wa ndege nilipokelewa na askari wenye silaha za moto nikajiuliza maswali mengi sana kuhusu amani tuliyonayo hapa Tanzania "alisema Malisa

Hatahivyo, alitoa wito kwa serikali kuunga mkono juhudi za viongozi mbalimbali wa dini hapa nchini katika kuwasaidia vijana na kusema viongozi wa dini wanafanya kazi kubwa katika kuwainua watu kiuchumi na kuwaepusha na vitendo viovu.

Awali akizungumza na waandishi wa habari mchungaji wa kanisa la Ukombozi tawi la Arusha Mchungaji Ushindi alisema kwamba mhubiri huyo atakwenda kufanya huduma ya maombezi mkoani Arusha kwa siku nane na kuwataka wakazi hao kujitokeza kwa wingi.

Mchungaji Ushindi alisema kuwa wakazi wa jiji la Arusha wamepata neema kubwa ya kupata neno la Mungu kupitia mkutano huo wa maombezi .


Timu ya kwaya ikiwa inatumbuiza jukwaani katika viwanja vya reli jijini Arusha mkutano huo ni wa siku 8
Taswira ya watu waliojitokeza katika mkutano huo
Kulia ni mama mchungaji Grace Mshindi wa kanisa la ukombozi tawi la Arusha akiwa anazungumza na watu waliojitokeza katika mkutano huo wa maombezi na kupokea uponyaji

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni