.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 21 Oktoba 2016

PAUL POGBA AANZA MAKALI YAKE WAKATI MANCHESTER UNITED IKISHINDA


Kiungo Paul Pogba amefunga mara mbili wakati Manchester United ikipata ushindi mrahisi wa magoli 4-1 dhidi ya Fenerbahce na kukwea hadi nafasi ya pili katika kundi A, katika mchezo wa Ligi ya Uropa.

Huku ikimrejesha dimbani, Wayne Rooney, Manchester United haikuwa na madhara sana hadi pale Fenerbahce ilipotoa penati mbili za kizembe.

Pogba alifunga goli la kwanza baada ya Simon Kjaer kumchezea rafu Juan Mata na baadaye Anthony Martial kufunga penati ya pili baada ya kusukumwa na Sener Ozbayrakli.

Pogba aliyeweka rekodi ya uhamisho alifunga la tatu kwa shuti zuri la mpira wa kuzungusha kutoka umbali ya yadi 20, na kisha Jesse Lingard kufunga la nne katika umbali kama huo.
                        Paul Pogba akiachia shuti lililozaa goli la tatu la Manchester United
 Mchezaji wa zamani wa Manchester United Robin van Persie akifunga goli pekee la Fenerbahce

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni