.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 22 Oktoba 2016

PENATI YA DAKIKA ZA MWISHO YA LIONEL MESSI YAIPATIA BARCA USHINDI

Lionel Messi amefunga penati katika dakika za majeruhi na kuisaidia Barcelona kutoka nyuma dhidi ya Valencia na kuibuka na ushindi wa magoli 3-2 wakiwa ugenini na kuongoza ligi ya La Liga.

Katika mchezo huo Messi aliipatia Barcelona goli la kuongoza lililozua utata, baada ya Luis Suarez aliyekuwa ameotea kuuruka mpira wa chini aliokuwa ameupiga na kujaa wavuni.

Valencia walipambana na kupachika magoli mawili kupitia goli la jitihada binafsi la Munir el Haddadi na Rodrigo kuongeza la pili, lakini Suarez alisawazisha na Messi kufunga la tatu.
                 Lionel Messi akiachia shuti la mkwaju wa penati ulioipatia ushindi Barcelona 
Wachezaji wa Barcelona Neymar na Suarez wakiwa chini baada ya kupigwa na chupa na mashabiki wa Valencia wakati wakishangilia goli la ushindi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni