.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 28 Oktoba 2016

RAIS WA PHILIPPINE RODRIGO DUTERTE ASEMA AMEMUAHIDI MUNGU KUACHA LUGHA CHAFU

Rais wa Philippine Rodrigo Duterte amesema kuwa amemuahidi Mungu kuwa atajaribu kuachana na tabia yake ya kuwa na mdomo mchafu unaomfanya kutoa lugha chafu kwa viongozi wenzake.

Rais Duterte ambaye ni maarufu kwa kutoa lugha chafu kwa viongozi wenzake, ametoa kauli hiyo wakati akiwasili katika mji wa nyumbani kwao wa Davao baada ya kufanya ziara ya Japan, na kusema Mungu amemtaka kuachana na tabia ya lugha chafu alipokuwa kwenye ndege.

Nikiwa angani nilisikia sauti ikiniambia kuwa acha tabia ya kutoa lugha za matusi ama ndege itaanguka, na ndipo nilipomuahidi Mungu kuwa ataacha kabisa kutukana,” alisema rais Duterte.

Duterte aliwahi kumuita rais Barack Obama mtoto wa kahaba, na kuuita Umoja wa Ulaya kuwa ni umoja wa kinafiki, pia alitishia kujitoa Umoja wa Mataifa kwa kumfananisha na Hitler, baada ya kusema angejisikia faraja kuwauwa wafanyabiashara wa dawa za kulevya milioni tatu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni