.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 27 Oktoba 2016

REAL MADRID YAFANYA KUFURU KWA KUISHUSHIA MVUA YA MAGOLI LEONESA

Timu ya Real Madrid imeishushia kipigo cha paka mwizi timu ndogo ya daraja la tatu ya Cultural Leonesa kwa kuichakaza kwa magoli 7-1 katika mchezo wa kombe la Copa del Rey.

Katika mchezo huo ambao Madrid waliwapumzisha Cristiano Ronaldo, Gareth Bale na Karim Benzema, walipata goli la kwanza baada ya mchezaji wa zamani wa West Brom beki Gianni Zuiverloon, kujifunga

Magoli mengine ya Real Madrid yalifungwa na Marco Asensio na Alvaro Morata waliofunga magoli mawili na Nacho na Mariano walifunga moja kila mmoja.
                 Gianni Zuiverloon akiwa amempoteza mahesabu kipa wake na kujifunga 
                                                     Marco Asensio akifunga goli la pili la Real Madrid

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni