.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 7 Oktoba 2016

TIMU YA TAIFA YA ITALIA YALAZIMISHA SARE DHIDI YA HISPANIA

Italia imepambana na kuambulia sare ya goli 1-1 katika mchezo wa kuwania kufuzu kutinga michuano ya kombe la dunia 2018 dhidi ya Hispania kupitia penati ya dakika za mwisho ya Daniele de Rossi.

Katika mchezo huo uliochezwa nchini Italia Hispania iliutawala mchezo kwa asilimia 72.4, katika kipindi cha kwanza lakini ilishindwa kufumania nyavu.

Hispania ilipata goli lake katika dakika ya 55 baada ya kipa mkongwe Gianluigi Buffon kushindwa kuokoa mpira na kumpa fursa Vitolo ya kuutumbukiza mpira wavuni.
                    Kipa Buffon akifanya kosa ambalo lilimfanya Vitolo kupachika goli 
             Mchezaji De Rossi akigugumia maumivu baada ya kugongwa na mguu wa Diego Costa
                        Daniele de Rossi akipiga penati iliyoisawazishia goli Italia na kutoa sare

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni