.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 27 Oktoba 2016

WAZIRI MBARAWA APOKEA RIPOTI YA AWALI YA UPIMAJI WA MIPAKA KATIKA KIWANJA CHA NDEGE CHA KIA.

rep1
Mtaalam wa kurusha roboti ya ndege (Drone) kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) (Watatu kushoto), Bw. Fredrick Mbuya akitoa ufafanuzi wa namna zoezi la kupiga picha katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) lilivyotekelezwa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza Kulia). Hatua hiyo itaiwezesha Serikali kumaliza mgogoro wa ardhi kati ya KIA na wananchi katika eneo hilo.
rep2
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, akikagua roboti ya ndege (Drone) iliyotumika katika zoezi la kupiga picha katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Kushoto ni Katibu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Vallery Chamulungu.
rep3
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, akifatilia kwa makini maelezo ya Mtaalam wa kurusha roboti ya ndege (Drone) kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Fredrick Mbuya, wakati akipokea taarifa ya awali kuhusu zoezi la kupiga picha katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
rep4
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dkt. Hassan Mshinda akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa ramani ya eneo la uwanja wa ndege wa KIA, baada ya zoezi la kupiga picha kukamilika.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni