.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 26 Novemba 2016

BONDIA DAVID HAYE NA TONY BELEW KUZIDUNDA MACHI MWAKANI

Bondia David Haye na Tony Bellew wametia saini makubaliano ya kupigana katika pambano la ngumi la uzito wa dunia Jijini London mwakani.

Mabondia hao watapanda ulingoni katika dimba la 02 Machi 4 mwakani baada Bellew bingwa wa dunia uzito wa cruiserweight, kujipandisha daraja ili apambane katika uzito wa juu.

Bellew alisisitiza kuwa anataka kupambana na bingwa huyo wa zamani wa uzito wa juu, tangu ashinde mkanda wa WBC cruiserweight katika majira ya joto.
                         Tony Belew akimdunda BJ Flores katika pambano la uzito wa cruiserweight
                 David Haye akimdunda Arnold Gjergjaj baada ya kurejea tena ulingoni mwezi Mei

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni