.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 21 Novemba 2016

DIEGO COSTA AIPANDISHA CHELSEA KILELENI MWA LIGI KUU YA UINGEREZA

Goli la kumi la Diego Costa katika msimu huu limeiwezesha Chelsea kukwea kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza na kuizamisha Middlesbrough katika dimba la Riverside kwa ushindi wa goli 1-0.

Chelsea ambayo hadi sasa haijapoteza michezo sita mfululizo ilianza kwa kasi katika mchezo huo mgumu na kufanikiwa kufunga goli pekee katika dakika ya 41.

Kocha wa Chelsea Antonio Conte amesema anashindwa kuamini ni kwa jinsi gani mabadiliko yanotoendelea katika timu yake yalivyopelekea kuongoza ligi.
 Shuti lililopigwa na Diego Costa kati kati ya msitu wa mabeki likimshinda kipa na kuelekea wavuni
         Kipa wa Middlesbrough akifanya kazi ya ziada kuokoa mpira uliopigwa na Pedro

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni