.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 16 Novemba 2016

HISPANIA YACHOMOA DAKIKA ZA MWISHO NA KUTOA SARE NA UINGEREZA

Mchezo wa nne wa kocha Gareth Southgate tangu apewe fursa ya kusaidia kuinoa Uingereza umeishia kwa sare ya aibu ya magoli 2-2 dhidi Hispania waliofunga mara mbili katika dakika za mwisho kwenye mchezo wa kirafiki katika dimba la Wembley.

Uingereza inayoonekana kuimarika tangu Southgate atwae mikoba ya Sam Allardyce walianza kufunga goli la kwanza kupitia kwa Adam Lallana kwa mkwaju wa penati ya mapema iliyotolewa baada ya kipa wa Hispania Pepe Reina kumuangusha Jamie Vardy.

Jamie Vardy aliongeza goli la pili akipiga kichwa cha chini cha kuchupa akiunganisha mpira wa krosi ya Jordan Henderson katika kipindi cha pili. Hispania ilisawazisha kupitia kwa Iago Aspas dakika ya 90 na Isco kufunga la pili dakika za nyongeza.
       Isco akifunga goli la kusawazisha kwa mpira uliompita tobo kipa wa Uingereza
                               Jamie Vardy akiruka kichwa cha kuchupa chini na kufunga goli
                                       Kipa Pepe Reina akimuangusha mshambuliaji Jamie Vardy

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni