.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 28 Novemba 2016

JOSE MOURINHO ATOLEWA NJE, MANCHESTER UNITED IKITOKA SARE


Kocha Jose Mourinho ametolewa nje kwa mara ya pili ndani ya mwezi moja wakati Manchester United ikitoka sare ya goli 1-1 na West Ham katika dimba la Old Trafford.

Kocha huyo Mreno alipiga teke chupa ya maji, katika kukerwa na uamuzi wa refa Jon Moss kumuonyesha kadi ya njano Paul Pogba kwa kujirusha.

Katika mchezo huo Manchester United ilijikuta ikifungwa dakika ya pili tu ya mchezo na Diafra Sakho akiunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu uliopigwa na Dimitri Payet.

Zlatan Ibrahimovic alisawazisha goli hilo katika dakika ya 21 kwa kuupiga kichwa mpira uliopingwa na Paul Pogba.
                Kipa David De Gea akiangalia wavuni mpira uliopigwa na  Diafra Sakho
               Zlatan Ibrahimovic akiruka juu na kuupiga mpira kichwa uliosawazisha goli
Guu la Zlatan Ibrahimovic likiwa juu na kuhatarisha usalama wa wachezaji wa West Ham

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni