.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 28 Novemba 2016

TIMU YA BARCELONA YABANWA NA REAL SOCIEDAD

Timu ya Barcelona itaingia wiki ijayo katika mchezo wa kwanza wa El Clasico katika msimu huu wakiwa pointi sita nyuma ya Real Madrid baada ya kutoka sare Real Sociedad.

Mabingwa hao ambao wameshindwa kupata ushindi katika dimba la Anoeta katika michezo yake minane, ilibidi wapambane kiume kusawazisha goli ili kuambulia pointi moja.

Alikuwa Willian Jose aliyewapatia wenyeji goli la kwanza katika mchezo huo, huku Gerard Pique akisaidia kuutumbukiza mpira kimiani wakati akijaribu kuuokoa.

Lionel Messi alichomoa goli hilo dakika sita baadaye na kufanya matokeo kuwa Real Sociedad 1-1 Barcelona.
              Lionel Messi akiachia shuti la guu lake la kushoto na kufunga goli la kusawazisha
    Luis Suarez akiwa ameshika kichwa baada ya Barcelona kufungwa goli la kwanza

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni