.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 30 Novemba 2016

KINDA BEN WOODBURN AVUNJA REKODI YA MICHAEL OWEN LIVERPOOL

Kinda Ben Woodburn amevunja rekodi ya Michael Owen ya kuwa mchezaji kijana mno kuifungia Liverpool na kuisaidia timu hiyo kuifunga Leeds United katika mchezo wa robo fainali ya kombe la EFL.

Wenyeji Liverpool wakiwa katika dimba la Anfield walipata goli lao la kwanza kupitia kwa mchezaji mwenye asili ya Kenya Divock Origi akitumbukiza kimiani mpira wa krosi ya winga wa kulia Trent Alexander-Arnold.

Liverpool walifanya matokeo ya mchezo huo kumalizika kwa magoli 2-0, pale kinda Ben Woodburn alipoandika historia mpya ya kuwa mchezaji kinda kuifungia goli Liverpool akiwa na umri wa miaka 17.
                                                        Divock Origi akiifungia Liverpool goli la kwanza 
Kinda Ben Woodburn akiachia shuti lililomshinda kipa wa Leeds United na kujaa wavuni

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni