.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 5 Novemba 2016

SUNDERLAND YAUONA MWEZI KWA MARA YA KWANZA LIGI KUU YA UINGEREZA

Sunderland wakiwa wamebakia 10 uwanjani wamepata ushindi wao wa kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza katika msimu huu, wakati Jermain Defoe akifungwa goli la kipindi cha pili kwa mkwaju wa penati dhidi ya Bournemouth.

Matokeo hayo yalikuwa muhimu kwa timu hiyo inayojulikana pia kama Black Cats, ambayo ilionekana kuweka presha kubwa kwa wapinzani wao Bournemouth na kujikuta wakimpoteza Steven Pienaar dakika ya 59 aliyepewa kadi nyekundu.

Bournemouth walikuwa wa kwanza kupata goli katika dakika ya 11 ya mchezo huo wakati Dan Gosling alipounganisha mpira wa krosi uliopigwa na Adam Smith, na kufunga goli lake la tatu katika msimu huu, ambalo lilisawazishwa na Anichebe dakika ya 33.
          Kipa wa Sunderland akiwa hana la kufanya baada ya Dan Gosling kufunga goli
                       Anichebe akiisawazishia Sunderland katika dakika ya 33 ya mchezo huo 
          Jermain Defoe akifunga kwa mkwaju wa penati na kufanya matokeo kuwa 2-1

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni