Goli la mpira wa kichwa lililofungwa
na Marten de Roon katika dakika za majeruhi limeinyima ushindi
Manchester City katika dimba la nyumbani la Etihad, dhidi ya
Middlesbrough.
Katika mchezo huo mshambuliaji
Sergio Aguero aliifanya Manchester City kuwa mbele akitumbukiza
kimiani krosi ya Kevin de Bruyne na kufikisha idadi ya magoli 150
akiwa na Manchester City.
Middlesbrough iliimarika baada ya
mapumziko lakini Claudio Bravo aliokoa vyema mchomo wa Alvaro Negredo. Wakati kikosi cha Pep Guardiola kikiamini kinaibuka na ushindi
De Roon alisawazisha kwa mpira wa kichwa krosi ya George Friend
katika dakika ya 91.
Sergio Aguero akiangalia mpira alioupiga ukitinga wavuni na kuandi goli
Marten de Roon akiwa ameruka juu kupiga mpira wa kichwa ulioandika goli la kusawazisha
Mpira wa kichwa uliopigwa na Marten de Roon ukimshinda kipa Claudio Bravo




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni