.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 23 Novemba 2016

TIMU YA LEICESTER CITY YATINGA 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA

Timu ya Leicester City imeendeleza mwenendo mzuri katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na kutinga hatua ya mtoano baada ya kuifunga Club Brugge kwa magoli 2-1.

Katika mchezo huo Leicester City ilikuwa inahitaji pointi moja tu kutinga hatua ya 16 bora lakini ikapata pointi tatu zitakazo wahakikishia kumaliza wakiwa vinara katika kundi G.

Shinji Okazaki alifunga goli safi la kwanza akiunganisha krosi ya Christian Fuchs, huku Riyad Mahrez akifunga goli la ushindi kwa shuti la penati, Jose Izquierdo alifunga goli pekee la Club Brugge.
                      Mpira uliopigwa na Shinji Okazaki ukitinga wavuni na kuandika goli
            Riyad Mahrez akifunga goli la pili la Leicester City kwa mkwaju wa penati
Tottenham imetolewa katika Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuzidiwa kabisa kisoka na Monaco katika dimba la Stade Louis II na kufungwa magoli 2-1.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni