Wanafunzi wawili wa Chuo Kikuu
wamekamatwa katika kituo cha kufanyia mitihani kwa wanafunzi binafsi
cha Makadara, Jijini Nairobi baada ya kukutwa wakiwafanyia Mitihani wa Taifa
wa Sekondari wengine.
Mmoja wa watuhumiwa Alice Ahunyes,
alikuwa anamfanyia mtihani Scholastica Wanjiru mwenye nambari ya
mtihani 2090101144 ambaye ni mfanyabiashara aliyeenda Ghana kununua
bidhaa za duka lake.
Mtuhumiwa mwingine, Salome Ondusa
ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kenyatta, alilipwa shilingi
10,000 na mwanafunzi binafsi Anne Erastus mwenye namba ya mtihani 2090101177 ili amfanyie mtihani.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni