.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Novemba 2016

YAYA TOURE AREJEA DIMBANI KWA KISHINDO NA KUIPATIA USHINDI MANCHESTER CITY

Yaya Toure amerejea kwa kishindo uwanjani kwa kuifungia Manchester City magoli mawili na kuipatia ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Crystal Palace.

Toure, akicheza kwa mara ya kwanza katika ligi kuu ya Uingereza kwa msimu huu baada ya kumaliza tofauti zake na kocha, alishirikiana vyema na Nolito na kufunga goli la kwanza.

Hata hivyo Crystal Palace walijibu mapigo na alikuwa Wilfried Zaha aliyemtengenezea nafasi Connor Wickham aliyetokea benchi na kusawazisha goli.

Hata hivyo Toure, ambaye hakuwa na City kwa takriban miezi mitatu alipachika goli la pili akiutumbukiza kimiani mpira wa kona uliopigwa na Kevin de Bruyne.
                        Yaya Toure akishangilia goli baada ya kutikisa wavu wa Crystal Palace 
                 Connor Wickham akifunga goli pekee la Crystal Palace katika mchezo huo 


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni