.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 1 Desemba 2016

MANCHESTER UNITED YACHARUKA KOMBE LA EFL NA KUTINGA NUSU FAINALI

Manchester United imetinga kirahisi nusu fainali ya kombe la EFL, baada ya kuichakaza West Ham kwa magoli 4-1, huku kocha wao akitumikia adhabu ya kufungiwa mechi moja.

Katika mchezo huo Zlatan Ibrahimovic alikuwa wa kwanza kufunga goli katika dakika ya pili tu ya mchezo kabla ya kinda wa zamani wa United, Ashley Fletcher kusawazisha goli hilo.

Anthony Martial alifunga goli la pili la Manchester United mara tu baada ya kuanza kipindi cha pili akiunganisha pande alilopigiwa na Henrikh Mkhitaryan.

Martial tena akaufunga goli la tatu kufuatia krosi ya chini iliyopigwa na Antonio Valencia kufuatia shambulizi lililopangwa vizuri, kabla ya Ibrahimovic kufunga goli la nne.
                                  Zlatan Ibrahimovic akielekea kufunga goli la kwanza katika mchezo huo 
             Zlatan Ibrahimovic licha ya kufunga goli hilo alikumbana na dhahama hii
                                Anthony Martial akifunga goli katika mchezo huo wa jana usiku

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni