.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 8 Desemba 2016

TOTTENHAM YAFANIKIWA KUTINGA HATUA YA MTOANO LIGI YA MABINGWA ULAYA

Timu ya Tottenham Hotspur imefanikiwa kufuzu kutinga hatua ya mtoano katika Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya timu ya CSKA Moscow ya Urusi.

Spurs, ilikuwa inahitaji kuepuka kipigo ili kumaliza katika nafasi ya tatu katika kundi F, ilikuwa ya kwanza kufungwa goli na Alan Dzagoev lakini goli hilo lilisawazishwa na Dele Alli.

Harry Kane alifunga goli la pili, kabla ya goli kipa wa CSKA, Igor Akinfeev kuizawadia Spurs goli kwa kuuelekezea ndani ya goli lake mpira wa kichwa uliopigwa na Alli wakati akijaribu kuuokoa.
                                        Dele Alli akipiga mpira uliozaa goli la kwanza la Tottenham
                                       Mshambuliaji Harry Kane akifunga goli la pili la Tottenham 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni