.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 8 Desemba 2016

MARCO REUS AIOKOA BORUSSIA DORTMUND ISILALE DHIDI YA REAL MADRID

Marco Reus amefunga goli la kusawazisha katika dakika 88, na kuipatia Borussia Dortmund sare ya magoli 2-2 dhidi ya Real Madrid, na kuihakikishia kumaliza kinara wa kundi F katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Katika mchezo huo mshambuliaji Mfaransa Karim Benzema alifunga magoli yote mawili la kwanza katika kipindi cha kwanza na la pili kipindi cha pili na kuifanya Real Madrid kuonekana kuutawala mchezo huo.

Mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang alichomoa goli la kwanza katika dakika ya 60, kabla ya Marco Reus kufanya mchezo huo umalizike kwa sare.
                    Karim Benzema akifunga bonge la goli kwa kuruka kichwa cha nguvu 
                            Pierre-Emerick Aubameyang akifunga goli la kwanza la Dormund 
                   Marco Reus akifunga goli la kusawazisha akimpoteza kipa Keylor Navas

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni