.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 12 Desemba 2016

WEST HAM YAPAMBANA KIUME NA KUIWEKEA NGUMU LIVERPOOL

Magoli yaliyofungwa na Dimitri Payet na Michail Antonio yameanika uzaifu wa beki ya Liverpool, wakati West Ham ikijikwamu kutoka kwenye mstari wa kushuka daraja kwa kuambulia sare ya magoli 2-2 katika dimba la Anfield.

Baada ya kufungwa magoli 4-3 na Bournenouth wiki iliyopita, Liverpool ilijikuta ikifungwa magoli mawili katika kipindi cha kwanza tu cha mchezo yaliyofungwa na Payet na Antonio.

Katika mchezo huo Liverpool ilipata goli la kwanza kupitia kwa Adam Lallana katika dakika ya tano ya mchezo , na kisha kupata goli la kusawazisha kupitia kwa Divock Origi katika kipindi cha pili.
                Dimitri Payet akipiga kiufundi mpira wa adhabu ulioenda kujaa wavuni 
Mshambuliaji mwenye asili ya Kenya Divock Origi akiifungia Liverpool goli la kusawazisha

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni